Event Details
Photo

Posted: 2025-12-18

WAZIRI WA KILIMO UMWAGILIAJI MALIASILI NA MIFUGO AWASHAJIHISHA WAFUGAJI WA KUKU ZANZIBAR

Description

Waziri wa Kilimo Umwagiliaji Maliasili na Mifugo Zanzibar Suleiman Masoud Makame amesema wataendelea kuwashajihisha  na kuwaunga mkono wafugaji wa kuku  ili kuongeza hamasa ya  kuongeza  ufugaji wa kuku katika jamii 

\r\n\r\n

Ameyasema hayo wakati wa ziara ya kuwatembelea wafugaji wa kuku katika maeneo tofauti Wilaya  ya  Kaskazini na Wilaya ya kati Unguja ameeleza kuwa kwa wafugaji ambao wanauelewa mkubwa katika shughuli ya ufugaji ni vyema wakashirikiana na wafugaji ambao wanauhaba wa elimu ya ufugaji ili waweze kuzalisha  kitaalamu na kufikia  lengo

\r\n\r\n


\r\nAmesema uongezekaji wa ufugaji wa kisasa  nchini ni adhma ya Serikali kupitia Rais wa Zanzibar Dk Hussein Ali Mwinyi  ya kuongeza upatikanaji wa chakula cha uhakika kwa Zanzibar na kuacha ufugaji wa kimazowea na kufuga ufugaji wa kisasa ili kuinua pato la Taifa sambamba na upatikanaji wa ajira kwa wananchi 

\r\n\r\n

Aidha kwa upande wa Naibu Waziri wa kilimo Umwagiliaji Maliasili na Mifugo Zanzibar Dr. Salum Soud Hamed amesema kuna muelekeo wa ufugaji mzuri  wa ufugaji wa kisasa na kibiashara na wenye tija kwa kushirikiana na Bank ya Maendeleo ya kilimo (TADB) ambao wamekuwa wadau wakubwa wa Maendeleo katika sekta ya kilimo kwa kuwapatia mikopo wafugaji sambamba na utowaji wa elimu ili kufuga kwa kupata faida

\r\n\r\n

Amesema lengo la Bank hiyo ni kuona wafugaji wanapata maendeleo na kujitatua kiuchumi ameeleza kuwa kwa upande wa Wizara ya Kilimo ni faraja kuwa na wadau wanawaunga mkono wafugaji na kuwaona wafugaji wanasimamia vyema fursa zilizopo 

\r\n\r\n


\r\nAidha kwa upande mwengine amewataka wafugaji wengine ambao bado  hawajaingia katika ufugaji wa kisasa na wenye tija wafike katika idara ya Maendeleo ya Mifugo kupatiwa maelekezo ili na wao waweze kufuga ufugaji wa kisasa  ili kufikia dhamira ya Serikali kuwainua wananchi kiuchumi na kufikia malengo waliojiwekea 

\r\n\r\n

Kwa upande mwengine ameeleza kuwa ufugaji wa kuku utaweza kuwapatia ajira na kupata usalama wa chakula nchini amesema upo uhitaji wa kuku jambo ambalo litapelekea upatikanaji wa fursa za  soko  ya uhakika  wa bidhaa zitokanazo wa uzalishaji wa kuku hao 
\r\nAidha kufuata utaratibu wa ufugaji ili  kufuga kiusalama na kuweza kuzalisha mayai yenye ubora na siha kwa watumiaji na kupata masoko ya kitaifa na yakitali .

\r\n\r\n


\r\nKwa upande wake Mkurugenzi Idara ya Maendeleo ya Mifugo Zanzibar Asha Zahran Mohammed amesema mkakati wa Idara ni kuwafikia wafugaji wote kuwapatia elimu ili waondokane na ufigaji wa kimazowea na kufuga ufugaji wa kibiashara ili kuongeza udhalishaji kwa wingi na kufikia ufugaji wa kibiashara 

\r\n\r\n

Amesema matarajio yapo makubwa ya kuongezeka kwa udhalishaji wa ndani  wa mayai kutokana na kuwepo kwa wafugaji wanaozalisha kwa siku trea 250 za mayai na kuongeza zaidi ya kiwango hicho kwa siku ili tuweze kujitosheleza nchini na kuacha  uagizishaji wa mayai kutoka nje ya Zanzibar 

\r\n\r\n

Amesema kwa ya Idara ya Maendeleo ya Mifugo ina  takwimu zinaonesha uzalishaji wa kuku  wa yai kwa hapa  Zanzibar umefikia asilimia  70 ukilinganisha na apo awali kwa kushirikiana na bank ya maendeleo kilimo kwa kutoa mikopo  kwa wafugaji wa kuku wa yai 

\r\n\r\n

Kwa upande wa Afisa biashara kutoka Bank ya Maendeleo ya Kilimo (TADB) Abio  Ntakisigaye amesema  wanafaraja kutokana na ziara hiyo itapelekea  kuongeza juhudi  za wafugaji na kuongeza uzalishaji na kuweza kusaidiwa na Serikali .

\r\n\r\n

Amesema Bank ya maendeleo ya kilimo haipo katika utowaji   mikopo  inajishuhulisha na utowaji wa elimu ili kuhakikisha wanaweza kutatua matatizo yanayojitokeza kwenye miradi  yanaweza kutafutiwa ufumbuzi na kuweza kupata maenedeleo mazuri katika jamii.

\r\n

Follow Us